Japan imepanga kuleta ushindani katika malipo ya Apps yaliyotawaliwa na Apple na Google


 Japan inapanga kuongeza ushindani katika malipo ya ‘apps’ za simu janja, inayotawaliwa na Apple na Google, kwa kupiga marufuku ‘major App store operators’ kutumia mifumo ya Apple na kuwalazimisha watengenezaji wa Apps kutumia mifumo ya malipo yao wenyewe, jopo la serikali lilisema, kulingana na Reuters.

 Ripoti ya mwisho ya jopo hilo, iliyotolewa Ijumaa, pia ilisema wasambazaji wakuu wa mifumo ya uendeshaji ya simu janja (Smartphone Operating Systems) wanapaswa kulazimika kuwapa watumiaji njia mbadala za kupata apps kwa njia salama mbali na ‘App Store zao’

IOS ya Apple na Android kutoka kwa Alfabeti ya Google ziligawanya soko la ‘Smartphone operating systems’ la Japani.

Apple huruhusu watumiaji kupakua Apps za iPhone kupitia ‘App store’ pekee, lakini pia Apple na Google zinahitaji ‘software developers’ kutumia mifumo ya malipo ya wamiliki ambayo hutoza kamisheni ya hadi 30%.

Ripoti hiyo ilisema kwamba hatua muhimu za kisheria zitaangaliwa wakati ujao, wakati Asahi Shimbun iliripoti Jumamosi kwamba serikali inalenga kuwasilisha mswada husika bungeni mapema mwaka ujao.

Wajumbe wa jopo la serikali ni pamoja na Waziri wa Viwanda Yasutoshi Nishimura na Waziri wa Uchumi Shigeyuki Goto.